0
Ng’ombe hazeeki maini, Lukas Mkenda aka Mr.Nice bado anaendelea kukimbiza Kenya japo nyumbani kwasasa hasikiki kabisa.


Muanzilishi huyo wa ‘Takeu style’ amesema amepata shavu la kupiga show 47 nchini Kenya, shavu alilopewa na kampuni ya Ki’nigeria,


“Niko huku Kenya,kuna kampuni ya Nigeria imenipa dili la kufanya tour kwenye county zote za Kenya, ziko 47″ Mr. Nice aliiambia Radion one.

Pia Mr.Nice amesema ana project mpya na Jaguar na Wyre ambazo zitatoke hivi karibuni,

“Pia nina project na wasanii wengine wa Kenya ambao wameniomba nifanye nao kazi,tuko na project na Jaguar na nyingine na Wyre kwa hiyo soon mambo yatakuwa mazuri”

Post a Comment

 
Top