Mmmmm….!!!
Kila nikiangalia picha hii
najikuta tu nahama kimawazo, nauli yangu ni maswali nasafiri kifikra hadi
stendi kuu ya chozi iliyopo Rhotia Karatu ambapo naongezewa nauli ya kurudi May
6, 2017.
Ndugu zangu, washiriki wa Madini Media, kwanza kabisa
nitoe pole kwa wote walioguswa na jambo hili, huku nikiwasihi kufuta machozi
kila mmoja kwa leso yake maana huwezi jua, wenda ya mwenzio
ina pilipili.
Shukrani
zangu za pekee ni kwao wote waliofanikisha kuisitiri miili ya wenzetu katika
nyumba maalumu, kama heshima anayostahili kila mwanadamu pindi anapomaliza
safari yake ya hapa duniani.
Wakati
naandika haya mmoja akasema, “Hili la ajari limepitwa
na wakati…” sikutaka kuongelea hizo habari zake ili asije
akaelewa, nachoshangaa naye ni mwandishi, nachoshukuru si wa Media hii maana angetutia hasara.
Linapotokea
jambo zito kama hili hakuna ulazima wa kukimbizana ku-copy na ku-pest habari za
hivi punde ‘breking news’ kwa raia
badala ya kukimbizana katika ofisi mbalimbali za kuweza kutoa
msaada wa haraka.
Kwa
sababu hamkupata kutoa ya moyoni kupitia hii media ambayo wengi mnapachukulia
kama nyumbani, basi leo nakupa hiyo fursa kupitia comments lakini kwanza
nikushirikishe machache ninayotafakari hata sasa:
⇗Vifo 35 Ni Shangwe Fb Na Insta.
⇗Kauli za kikatili kutoka tabaka la juu.
⇗Thamani ya misiba katika vyombo vya habari.
⇗Muarobaini…!!!
Kwa
wale wenzangu wenye bifu na maandishi wanatamani niishie hapo, weee… thubutu!
Lazima niendelee mpaka mwisho na nifafanue kila kimoja, na bila kuchoshana
tuanze na hii pointi ya kwanza.
⇛VIFO 35 NI SHANGWE FB NA
INSTA.
Asilimia
kubwa ya jamii walipokea hizi habari kupitia mtandao wa Facebook, na waliozipokea
kwa njia ya instagram pia ni wengi, kutokana kwamba hii mitandao inasifika sana
kwa picha na ni rahisi kuitumia.
Sema
kuna jambo nimegundua, yaani watumiaji wa mitandao hii wako speed kuliko muda
na ni majasiri hujawahi ona, hata hawatoi ufafanuzi zaidi ya kutupia tu picha
za miguu na vichwa vya watoto.
Mapokezi
ya picha hizi ni makubwa sana kutokana na maelfu ya watu walioonesha kuzipenda ‘likes’, kila mmoja akijitahidi kusema
chochote ‘comments’ na pendo katika
kushirikishana ‘shares’.
Hakika
hizi ni zama za swala kuwinda simba, mambo
yamebadilika, imefika wasaa binadamu wana roho za kinyama, imekuwa heri mara
mia mwanadamu kufanya urafiki na wanyama flani-flani
wana roho za utu.
Fanya
utafiti leo katika post zote zinazohusu ‘kuzuia ajali za
barabarani’ utakuta hazina likes
wala comments, kisha geukia hizi zinazoonesha vipande vya miili
utakuta zina mamia ya likes na comments.
Furaha
ya wana-fb na insta ni kuona matukio mabaya ya kusisimua, ila wana areji na
post zinazohusu mbinu za kujikinga na mabaya, ndio maana nikasema, “VIFO 35 NI
SHANGWE FB NA INSTA”
⇛KAULI ZA KIKATILI KUTOKA TABAKA
LA JUU.
Naskia
baba yenu kasema wanahabari hawana uhuru kama
wanavodhani, ila hii kauli sidhani kama inanizuia kutoa pole kwa mwakilishi wa
jimbo la Arusha mjini kwa msiba huu maana unamgusa moja kwa moja.
Tuliokuwepo
wakati wa kuaga miili tulimwona na tulitaraji ataongea chochote lakini ikawa
tofauti, kumbe mama yenu aligoma kumpa nafasi, hata kaka Mbowe alipomkumbusha
mama bado juhudi ziliangukia ziro.
Ni
mengi yameongelewa kuhusiana na hili pigo tulilopata, wenye busara zao na hata
vifata upepo wote wameonesha ushirikiano katika kuishauri serikali ili ikiwezekana
jambo kama hili lisitukie tena hapa nchini.
Hoja
zenu za msingi naamini wahusika watazifanyia kazi kwa kadri mlivyowaamini hata
kuwapa dhamana ya pale walipo, ila nina neno juu yao kuhusiana na kauli
walizokuwa wakitoa, na hizi ni baadhi:-
- Wanafunzi ni taifa la kesho.
Watu
wengine bwana, Mungu awasamehe tu maana hawajui wayanenayo, au mmesahau kuwa
uzima na mauti u kinywani mwenu, kinywa huumba, leo unatamka kuwa thamani ya
wanafunzi itaonekana kesho.
Ndio
maana hata hamjali usalama wao leo, kachunguze vyakula, mahari wanapolala, gusa
na nidhamu, ukitoka huko ingia kwenye school bus, kuna wakati utakutana na
benchi ndio siti, na dreva lazima awe ndugu.
Serikali
ya viwanda lazima iwe makini hasa kwa hawa wanafunzi tunaowategemea baadae,
serikali ya vibanda ndio wakati wowote inaweza kuharibiwa kwa upepo na kuleta
mauaji kutokana na udhaifu wa misingi yake.
- Kupunguza ajari.
Kuna
kipindi nawaza mpaka nachukia, yaani na hiyo mikakati yote ya usalama
barabarani, majumbani, viwandani, mashuleni, mahospitali na kwingineko, kumbe
nia na madhumuni ni kupunguza ajari, kupunguza tu!
Bajeti
kubwa inatengwa kwa ajili ya kulipia matangazo katika vyombo mbalimbali vya
habari, kununua air-time redioni, show-time katika runinga na space katika
machapisho, kumbe yote hayo ni mbinu za kupunguza tu.
Unaweza
kupunguza ajari 9 kati ya 10 (90%), ila hiyo moja tu uliyoiruhusu ikaandika
historia kubwa kuliko hii, sitaki kumfundisha kazi awaye yote ila nachoamini
kuwa bora ni mbinu za kuzuia ajari na sio kupunguza tu.
- Msiba wa kitaifa.
Nakumbuka
sana eneo hili la tukio, maana ndipo alipopatia ajari babu na bibi wakiwa
wamebebana kwenye baiskeli wakitoka hospitali na wote wakafa, sikuskia habari
za uchunguzi maana huo ulikuwa ni msiba wa kiukoo tu.
Maisha
ya A yaliishia pale pale kwa pikipiki, akafata B akiwa na NOAH, hawa wote ni
ndugu, na tabaka la juu halikuongea chochote kwa sababu haihusiani na taifa,
tulipojaribu kuomba msaada tukaambiwa ni msiba wa kifamilia.
Leo
chunusi imegeuka jipu ndio mnakimbizana kusimika bendera ya taifa, kisa msiba
wa kitaifa, kivipi wakati mwakilishi wa taifa katika eneo hilo alinyimwa nafasi
ya kutoa hata pole, maslahi binafsi bifu hadi msibani, waone!
⇛THAMANI YA MISIBA KATIKA
VYOMBO VYA HABARI.
Utakubaliana
nami kuwa kazi kuu tatu za vyombo vya habari ni kuhabarisha,
kuelimisha na kuburudisha jamii,
ila kwa media za kibongo ni nadra sana tangu mamluki walipovamia hii tasnia kwa
masilahi yao binafsi.
Tabaka
la juu katika hii tasnia kumejaa
kukuru-kakara hadi nguo ikachanika mmoja katishiwa bastola, aliyenunuliwa
nguo mpya ndio kwanza haielewi ni ya kike au ya kiume, usimuulize, sababu nguo ni nguo na tayari katokelezea.
Tabaka
la chini wamekula chunvi nyingi
katika darasa la hii tasnia, leo wanadai ni muda wao sasa wa kulamba sukari,
wanaisaka kwa udi na uvumba, kwa njia halali na hatari wao wamo tu mradi ulimi uguse kiganja.
Mpaka
kesho wasaka kiki katika media wanajua, hakuna kiki kubwa kuliko kufa, maana
hapo kazi zako zitasapotiwa bila gharama, hata mdogo wako wa mwisho atafanyiwa
interview, any way, tuangazie baadhi ya media.
- Milard Ayo
Huyu
kijana anasifika ndani na nje ya nchi kutokana na bidii zake katika kutoa
habari za haraka na makala zenye ukweli na usahihi, zinazogusa jamii na
anatajwa kuwa changamoto kwa wanahabari wa Tanzania.
Nilipoona
picha za ajari fb, nikakimbilia kwenye blog yake nipate ufafanuzi zaidi, ndio
kwaaaza kabadilisha front view kajaza picha na habari za Frola mbasha kusifiwa
na mume wake mpya na picha za hamo-wolper.
Sababu
namuamini nikaanza kufuatilia posts, sasa yeye kazidi wote kwa post za vipande
vya miili ya watu, ndo nikajiuliza ni chuo gani alichosoma huyu jamaa hata
hajui sheria, sera na maadili ya uandishi wa habari.
- Bongo5
Baada
ya kaka yenu kunichanganya ikabidi nisitoke haraka mtandaoni bali nipitie na
blog nyingine sababu naamini kuna wanahabari wengi wanafanya poa kuliko yeye,
ndo nikaangukia nyumbani Bongo kwa mara ya kwanza.
Kufunguka
tu nilipokelewa na matangazo ya makampuni makubwa-makubwa Tanzania, nikahisi
hapa ndio penyewe, kumbe ndio kwaaanza wanaungana na udaku kusema chanzo cha
ajari ni dreva kupigwa busu na mwanafunzi.
Siwezi
kumbuka niliumia kiasi gani nachokumbuka nilizima simu kwa zaidi ya siku, na
baadae sana nikafungulia redio nipate kuskiliza kuhusiana na taratibu za
mazishi, nikaanza na hawa wenye mitambo mikubwa.
- Clouds Fm.
Hii
ni redio ya kiburudani, nisijue kama ndio sababu ilikuwa radhi kusinzia siku
kadhaa ili zisirushwe habari za huzuni, au ndo vile kihamorapa tayari, nikae na
Samson Petter ‘Spy-D’ tumchunguze anayelia sana msibani.
Mbona
sijasikia habari za kufuliza siku kadhaa kwa ajili ya kutoa elimu juu ya
usalama wa watu na mali zao bila malipo, ili wasikilizaji wajielewe na kutambua
jinsi gani wanaweza kujiepusha na maafa yanayotukia kila siku.
Angelikuwa
mwanamziki ndio kafa, e eeee… ungeshuhudia hiyo shughuli yake anavopewa promo
na zitachezwa kazi zake hata alizoandaa akiwa kijijini sinazokoroma, zisizo na
ubora zinalembwa kama mwanamwali vile.
⇛MUAROBAONI.
Nikupongeze
kabisa ewe ndugu ulieketi nami jirani kwa kwa nia moja hata sasa, kwa umakini
ukipata hekima mbili tatu, katika machungu ukachukuliana nami nia na madhumuni
tufikie hapa ulipo muarobaini wa yote.
Changamoto nilizoainisha
ni chache sana kulinganisha na movie nzima ya kila siku tunayoshuhudia
vibandani, kwa habari ya viwanda wanajua wawekezaji na wakubwa, na kama utajitoa kuhoji pia uwe radhi kujitoa kitoweo.
Walipo wengi halishindikani jambo, mawazo yangu ni 1 ya 3 ya suluhisho,
nawe ukitoa 1/3 na yule 1/3 tayari 3/3=100% ya suluhisho itapatikana, basi
fanya hivo sasa kwa kukomenti maoni na ushauri wako kwa jamii nzima.
Asante
kwa kutembelea Madini Media, nakusihi sana kwa muda huu kagua vipengele
mbalimbali katika blog hii ili ujue mengi sana kuhusu maisha yako, na jitahidi
basi kila siku upitie hapa uone tumekuandalia nini.
©M(F)25MA17-03
Author: Fiacrius K. Otto
Editor: Samson P. Duttu
Allowed: Share, copy&paste
Don’t try: To edit any.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.